JINSI YA KUPIKA MAANDAZI

➡️ Karibuni maandazi, hapa na share recipe yangu ya maandazi, ambayo itakusaidia uweze kutengeneza maandazi mazuriii kwa urahisi na kuepuka kero ya kutafuta vitafunwa au kula mikate kila siku 😀.

➡️Recipe ya maandazi hii hapa 👇🏿
.
Mahitaji

Ngano kilo1, Mafuta lita 1, Sukari 200 gramu, Maji robo lita, Hamira vijiko 4 vidogo.

Jinsi ya kutengeneza

➡️ Weka maji kwenye bakuli yawe ya uvuguvugu kisha tia hamira koroga mpaka iyeyuke, kisha tia unga wa ngano katika bakuli kubwa ya kukandia, kisha tia sukari na mafuta kama vijiko vinne vikubwa katika unga, kisha tia maji uliyochanganya na hamira, anza kuukanda, kanda mpaka uone umechanganyika vizuri utengeneze donge moja kubwa.

Kisha baada ya kukanda acha kama dakika kumi na tano ngano yako, baada ya hapo ndio usukume na kukata shepu za maandazi unazotaka, acha yaumuke kama masaa mawili kisha kaanga. Unaweza kunywea chai maandazi au kinywaji chochote upendacho.

karibu kwenye comments kwa chochote kuhusu maandazi, pia usisahau ku follow blog ya malkia wa jiko, uweze kupata email kila napo post.

Kupata ratiba ya chakula ya mwezi mzima, ipo ktk soft copy tsh 10,000 Whatsap 0752 741 831.

Published by eunicemahundi

Hi🙋🏾, Naitwa Eunice Mahundi, ni #foodblogger na napenda sana mapishi, wengi mna nifahamu kama Mjasiriamali Ila food blogging ni kitu kingine nacho kipenda sana. 🍲🍝🍹🍷🍚🍽 Mapishi Yangu huwa ni simple, Ila yanavutia na mengi ni swahili cuisine, pia huwa napost dondoo za jikoni kama; -Usafi -vyombo -ratiba ya chakula/mapishi -nk Karibu sana na ione malkia wa jiko blog kama nyumbani kwako, ujifunze mengi. Ukiwa na maswali, maoni au chochote kile wasaliana nami: 📧 eunicemahundi@yahoo.com Whatsapp : 0752 741 831or 0657 234 897

13 thoughts on “JINSI YA KUPIKA MAANDAZI

      1. Mimi maandazi yangu yanakua na space kwa ndan japo nakata manene huwa sipendi nikiwa nachoma andazi lipande kama puto nifanyeje?

        Like

Leave a reply to Chiza Mtibuzi Cancel reply

Design a site like this with WordPress.com
Get started