➡️ Chapati za kusukuma; huwa napenda sana, ni tamua na hazina usumbufu wowote ktk kupika. Na uzuri chapati unaweza ukala wakati wowote iwe asubuhi, mchana au jioni. Hapa na -share recipe yangu ya chapati hope itawasaidia wengi;

Chapati recipe
Mahitaji
– ngano 1/2 kg
– mafuta 1/4 L
-chumvi kijiko kidogo 1
– maji 400 m/l

Jinsi ya kutengeneza
Weka maji kwenye kibakuli (400 M/l) yawe ya uvuguvugu kisha tia chumvi na koroga vizuri ichanganyike.
Tia unga wa ngano katika bakuli kubwa ya kukandia, kisha tia mafuta kama vijiko vinne vikubwa katika unga. Kisha tia maji katika unga na anza kuukanda, kanda mpaka uone umechanganyika vizuri utengeneze donge moja kubwa. Ukimaliza anza kutengeneza vidonge vidogo vya duara, kama kwenye picha kisha unavipanga kwenye kibao.

Kisha unachukua moja moja unasukuma, unaweka frying pan yako jikoni ukipata moto unaweka chapati, unaigeuza pande zote mbili ipate moto kisha unaweka mafuta unakaanga upande wa juu ukiwa tayari unageuza upande mwingine unaweka mafuta unaikaanga ukiwa tayari unatoa, unafanya hivyo mpaka zote zinaisha. 👇🏿
.

Chapati zako unaweza kula na chai, juisi au mchuzi wa nyama, maharage, mboga za majani au chochote utakachopenda.
.

➡️Kupata ratiba ya chakula ya mwezi mzima, ipo ktk soft copy tsh 10,000 Whatsap 0752 741 831.
asant kwa somo
LikeLike
karibu
LikeLike
Great recipe with best results
LikeLike
Thanks 🙏🏾🙏🏾
LikeLike
Asante kwa mafunzo mazur ya kupika
LikeLike
Karibu dear
LikeLike