
➡️Chicken Pilipili; huyu ni kuku wa kukaanga aliye tiwa pilipili na viungo vingine. Kama nilivyo sema kwenye post iliyo pita. Leo nita post, recipe ya #chickenpilipili. So ndio hii hapa,
➡️Mahitaji,

kuku wa kisasa 1(kl 1)
-pilipili mwendokasi 3
-pilipili mbuzi nyekundu3
-pilipili manga kjk 1 kikubwa
-binzari nyembamba1 kjk kikubwa
-kitunguu saumu 1,(toa maganda)
-tangawizi ya wastani (imenye)
-limao nusu
-chumvi kjk kdg 1
➡️Nilivyo tayarisha

- Baada ya kumwosha kuku, nika mkatakata vipande vya wastani. Na kumwacha pembeni achuje maji.
- Kisha nikachukua viungo vyote, nakuweka ktk kinu (kasoro limao na chumvi). Nika twanga hadi vika lainika.
- Nikachukua viungo na kuweka kwenye kuku, nikatia chumvi na kukamulia limao. Kisha nika mix vizuri kabisa ili viungo vienee ktk kila kila kipande cha kuku.
- Nikaacha kama nusu saa viungo vikolee ktk kuku, kisha ndio nika kaanga ktk mafuta, hadi kuku akawa brown. Nika toa nyama jikoni na ikawa tyr kuliwa.
- Hiyo ndio simple recipe ya kuku wa pilipili, ni mtamu sana anafaa kuliwa na chipsi, ndizi choma, pilau, ugali nk.
➡️Pilipili unaweza kuongeza au kupunguza, utakavyo penda.
➡️Kupata ratiba ya chakula ya mwezi mzima, ipo ktk soft copy tsh 10,000 Whatsap 0752 741 831.
