Juice ya ukwaju mix na ubuyu πΉ(tamarind baobab juice) kama hujawahi kunywa mchanganyiko wa juice hii basi uhondo una kupita. Ni juice(mix) tamu sana hasa ukila na nyama choma.
.

Mahitaji
ukwaju nusu kilo
ubuyu robo kilo
asali vijiko vikubwa 5
maji ya moto lita
Jinsi ya kutengeneza
Baada ya kutoa vyote kwenye maganda yake ni nika loweka ukwaju na ubuyu kwenye maji ya moto (maji niliweka lita 2). Nikauacha kwenye maji hadi maji yalipo poa kabisa, nikachukua mwiko na kuanza kukoroga ili ubuyu na ukwaju utoke kwenye maganda yake. Kisha nikachuja na kuweka asali na nikaweka juice Yangu kwenye fridge ipate baridi.
#Karibu
tembelea piaππΏ
https://eunicemahundi.wordpress.com
Ujifunze ujasiriamali