JINSI YA KUKAANGA VIPANDE VYA SANGARA

-Baada ya nyama kitu kingine nacho kipenda ni samaki, awe maji baridi au chumvi. Apikwe vyovyote vile mi nakula.❤️


-Hapa niliandaa vipande vya sangara . Baada ya kuosha vipande vya sangara i ni kakata vipande vidogo dogo, Kisha nikaacha vichuje maji.

Baada ya hapo, nikaanza kuweka viungo kama unavyo ona kwenye picha ;
-nimeweka curry powder kjk kikubwa 1
-pilau masala kjk kikubwa 1
-chumvi kjk kidogo 1
-garlic ginger paste kijiko 1 kikubwa
-limao kubwa 1


Kisha nikamix vizuri sana kwa kutumia mikono. Samaki na viungo vichanganyike vizuri. Halafu nikaweka samaki kwenye fridge kwa nusu saa viungo vikolee .


Baada ya hapo nikatoa na kukaanga kwenye mafuta kwa moto wa wastani, moto usiwe mkali sana. Samaki akatoka kakolee viungo, taste ni 🔥🔥 na ladha nzuri sana. Sangara wetu tulimla na ugali na kisamvu Cha nazi. #karibuni.


Wewe ungekula na Nini?? Share kwenye comments ❤️❤️❤️
Pia usisahau ku-subscribe, #malkiawajiko na kushare recipes zangu na uwapendao,thanks 🙏🏾

Published by eunicemahundi

Hi🙋🏾, Naitwa Eunice Mahundi, ni #foodblogger na napenda sana mapishi, wengi mna nifahamu kama Mjasiriamali Ila food blogging ni kitu kingine nacho kipenda sana. 🍲🍝🍹🍷🍚🍽 Mapishi Yangu huwa ni simple, Ila yanavutia na mengi ni swahili cuisine, pia huwa napost dondoo za jikoni kama; -Usafi -vyombo -ratiba ya chakula/mapishi -nk Karibu sana na ione malkia wa jiko blog kama nyumbani kwako, ujifunze mengi. Ukiwa na maswali, maoni au chochote kile wasaliana nami: 📧 eunicemahundi@yahoo.com Whatsapp : 0752 741 831or 0657 234 897

Leave a comment

Design a site like this with WordPress.com
Get started