JINSI YA KUPIKA ORANGE-RED CHICKEN

Orange red chicken: hii niliandaa weekend, kwa ajili ya lunch. Tulikula na ugali na kachumbari.

-Mapishi yake ni rahisi sana, baada ya kumuosha kuku na kumkatakata, nikamwekea;
-chumvi kidogo sn
-limao kjiko 1 kikubwa
-garlic ginger paste
-orange red powder kijiko 1 kikubwa.

Kisha nikamix vizuri, na mikono kuhakikisha kuku kakolea viungo. Halafu Nika chukua grill pan, na kuiwekea mafuta kidogo, Kisha nikaweka vipande vya kuku kwenye grill pan na kuiweka kwenye oven.

Nika set moto 150 degrees na kuoka kwa dk kama hamsini, kuku akawa tayari kama unavyo ona. Ila ukipenda unaweza mkaanga.

-Kuku akatoka mtamu sana, tulifaidi ugali. Wewe huyu kuku ungemla na nini?

share kwenye comments pia usisahau ku-subscribe #malkiawajikoblog.

Published by eunicemahundi

Hi🙋🏾, Naitwa Eunice Mahundi, ni #foodblogger na napenda sana mapishi, wengi mna nifahamu kama Mjasiriamali Ila food blogging ni kitu kingine nacho kipenda sana. 🍲🍝🍹🍷🍚🍽 Mapishi Yangu huwa ni simple, Ila yanavutia na mengi ni swahili cuisine, pia huwa napost dondoo za jikoni kama; -Usafi -vyombo -ratiba ya chakula/mapishi -nk Karibu sana na ione malkia wa jiko blog kama nyumbani kwako, ujifunze mengi. Ukiwa na maswali, maoni au chochote kile wasaliana nami: 📧 eunicemahundi@yahoo.com Whatsapp : 0752 741 831or 0657 234 897

Leave a comment

Design a site like this with WordPress.com
Get started