JINSI YA KUTENGENEZA PILIPILI YA EMBE

➡️Pilipili ya embe: Hii ni pilipili nzuri sana unaweza kula na vitu vingi nyama choma, chipsi, pilau, ndizi choma nk.


➡️Nimeweka -embe 1 bichi dodo kubwa, -pilipili mbuzi nyingi, -kitunguuu saumu 1, -tangawizi kiasi,
-Chumvi kijiko 1 kidogo
-majani ya rosemary kidogo
-na curry powder kidogo.

➡️Nimemenya embe na kuli katakata, nikamenya saumu,tangawizi, nikakatakata pilipili kisha nikaweka kila kitu ktk blender nikaweka pia na rosemary, na curry powder, vinegar kidogo na chumvi nika blender hadi mchanganyiko wangu ulipo kuwa laini, ila sikutaka uwe laini sana.


➡️Baada ya hapo nikweka mafuta jikoni yalipo pata moto, nika mimini pilipili yangu ktk mafuta na kukaanga kwa dk kadhaa, kidha nikazima jiko. Na kuacha pilipili ipoe. Halafu tukaila ni pilipili nzuri sana 😍.

Usisahau ku like, comment na ku share.

Published by eunicemahundi

Hi🙋🏾, Naitwa Eunice Mahundi, ni #foodblogger na napenda sana mapishi, wengi mna nifahamu kama Mjasiriamali Ila food blogging ni kitu kingine nacho kipenda sana. 🍲🍝🍹🍷🍚🍽 Mapishi Yangu huwa ni simple, Ila yanavutia na mengi ni swahili cuisine, pia huwa napost dondoo za jikoni kama; -Usafi -vyombo -ratiba ya chakula/mapishi -nk Karibu sana na ione malkia wa jiko blog kama nyumbani kwako, ujifunze mengi. Ukiwa na maswali, maoni au chochote kile wasaliana nami: 📧 eunicemahundi@yahoo.com Whatsapp : 0752 741 831or 0657 234 897

2 thoughts on “JINSI YA KUTENGENEZA PILIPILI YA EMBE

Leave a comment

Design a site like this with WordPress.com
Get started