SIMPLE BROWN CAKES

Simple chocolate cake recipe, ndio nayo penda kushare leo, ni recipe rahisi na post za nyuma niliwahi kushare kama hii tofauti tu yenyewe ilikuwa ni chocolate banana cake.

.

πŸ‘‡πŸΏ

Mahitaji
Ngano robo kilo
Baking powder vijiko vidogo 2
Sukari vijiko vikubwa 4
Mayai 2 (yaliyo pigwa pigwa tayari)
Cocoa powder 100gm
Siagi vijiko vikubwa 3
Maziwa 50ml .
Matayarisho
Niliwasha oven ianze kupata moto (160C). Kisha nikapasha siagi kwenye microwave nikaiweka pembeni. Nikawega unga kwenye bakuli, cocoa, sukari, baking powder, mayai na nika mix na mwiko hadi vikachanganyika vizuri, kisha nikatia siagi na maziwa huku naendelea mix hadi vikachanganyika vizuri.


(Kama unatumia mixer ni rahisi zaidi fanya kwa utaratibu huo huo) Kisha nikamimina mchanganyiko wangu kwenye chombo cha kuokea na kuweka kwenye oven, nikaoka dakika 55 cake ikawa tayari. Nilipika jana kwa ajili ya chai ya jioni.
.


#simplecake #simplechocolatecake cake #cakerecipe #yumyum #sweetcake #deliciousfood #gateau #gateauchocolat #keki #easyandsimple #eveningtea #snacks #tea #chai #kitchen #cooking #recipes #mapishi #jikoni #chakula #swipeleftπŸ‘ˆ #homebaking #gateauchocolat #rawcacaopowder #tanzanianblogger #jifunzemaishi #malkiawajiko #caketime

Published by eunicemahundi

HiπŸ™‹πŸΎ, Naitwa Eunice Mahundi, ni #foodblogger na napenda sana mapishi, wengi mna nifahamu kama Mjasiriamali Ila food blogging ni kitu kingine nacho kipenda sana. 🍲🍝🍹🍷🍚🍽 Mapishi Yangu huwa ni simple, Ila yanavutia na mengi ni swahili cuisine, pia huwa napost dondoo za jikoni kama; -Usafi -vyombo -ratiba ya chakula/mapishi -nk Karibu sana na ione malkia wa jiko blog kama nyumbani kwako, ujifunze mengi. Ukiwa na maswali, maoni au chochote kile wasaliana nami: πŸ“§ eunicemahundi@yahoo.com Whatsapp : 0752 741 831or 0657 234 897

Leave a comment

Design a site like this with WordPress.com
Get started