CHAPATI RECIPE

Chapati for dinner🍽: , mlo wa jioni inapendeza ukiwa unabadilisha vyakula kila siku, isiwe usiku kila siku ni wali tu, badilisha vyakula viazi, chapati, tambi, ndizi nk.
Recipe Yangu ya chapati ni simple na ya uhakika, mtag pia rafiki yako anaye penda chapati;


Chapati recipe
🍴
Mahitaji
πŸ‘‡πŸΏ
– ngano 1/2 kg
– mafuta 1/4 L
-chumvi kijiko kidogo 1
– maji 400 m/l
πŸ‘‡πŸΏ
Jinsi ya kutengeneza Weka maji kwenye kibakuli (400 M/l) yawe ya uvuguvugu kisha tia chumvi na koroga vizuri ichanganyike.
πŸ‘‡πŸΏ
Tia unga wa ngano katika bakuli kubwa ya kukandia, kisha tia mafuta kama vijiko vinne vikubwa katika unga. Kisha tia maji katika unga na anza kuukanda, kanda mpaka uone umechanganyika vizuri utengeneze donge moja kubwa. Ukimaliza anza kutengeneza vidonge vidogo vya duara, kama kwenye picha kisha unavipanga kwenye kibao. (angalia picha zinazo fata) πŸ‘‡πŸΏ
Kisha unachukua moja moja unasukuma, unaweka frying pan yako jikoni ukipata moto unaweka chapati, unaigeuza pande zote mbili ipate moto kisha unaweka mafuta unakaanga upande wa juu ukiwa tayari unageuza upande mwingine unaweka mafuta unaikaanga ukiwa tayari unatoa, unafanya hivyo mpaka zote zinaisha.πŸ‘‡πŸΏ
Chapati zako unaweza kula na chai, juisi au mchuzi wa nyama, maharage, mboga za majani au chochote utakachopenda.
.
.
.
.
#chapati #chapatirecipe
homecookingfood #simplerecipe #quickandeasyfood #africanfoods #africanfoodyummy #sweethome🏑 #africancooking # #foodfamily
.
. #tanzanianfood #foodbloggerlife #swahilifood #mapishi #jikoni #malkiawajiko #jifunzemapishi #jiko #tanzanianblogger #chakula #mapishiyakiswahili

Published by eunicemahundi

HiπŸ™‹πŸΎ, Naitwa Eunice Mahundi, ni #foodblogger na napenda sana mapishi, wengi mna nifahamu kama Mjasiriamali Ila food blogging ni kitu kingine nacho kipenda sana. 🍲🍝🍹🍷🍚🍽 Mapishi Yangu huwa ni simple, Ila yanavutia na mengi ni swahili cuisine, pia huwa napost dondoo za jikoni kama; -Usafi -vyombo -ratiba ya chakula/mapishi -nk Karibu sana na ione malkia wa jiko blog kama nyumbani kwako, ujifunze mengi. Ukiwa na maswali, maoni au chochote kile wasaliana nami: πŸ“§ eunicemahundi@yahoo.com Whatsapp : 0752 741 831or 0657 234 897

Leave a comment

Design a site like this with WordPress.com
Get started